“ Kilimo cha nanasi kinapendelea hali ya hewa ya joto na husitawi vema katika mwinuko kati ya mita 0-1750 kutoka usawa wa bahari. Mwinuko wa mita 1300 hadi 1750 hufaa zaidi kwa uzalishaji wa nanasi kwaajili ya kusindika na mwinuko chini ya hapo hufaa zaidi kwaajili ya ulaji wa moja kwa moja. Mahitaji ya joto ni kati ya nyuzi joto 18 °C hadi 35 °C. ” Utangulizi Nanasi ni tunda la kitropiki, linapendwa na walaji wengi kwa sababu ya ladha yake tamu na harufu yake nzuri. Tunda hili laweza liwa mara tu baada ya kuvunwa, baada ya kulipika, au kama juisi. Nanasi ni chanzo kizuri cha vitamin A na B, pia inakiwango kingi tu cha vitamin C pamoja na madini kama vile: patasiam, magnesiam, kalsiam, na madini chuma. Asili ya nanasi inaaminika kuwa ni Brazil na Paraguay huko Amerika ya Kusini. Hapa Tanzania, nanasi hulimwa zaidi maeneo ya Bagamoyo, Kibaha (Pwani), Tanga, Mtwara, Lindi, Geita na Mwanza. Lakini pia maeneo yote ya pwani ya Tanzania yanafaa kwa kilimo cha nanasi. Hali ya hewa Kilimo c...
“Matango huwa tayari kuvunwa kuanzia siku 50 hadi 60, yaani mwezi mmoja na nusu hadi miwili baada ya kupanda, na pia matunda yanatakiwa kuwa na urefu wa sentimita 15 mpaka 20, urefu pia unaweza kutofautiana kulingana na aina ya matango yaliyopandwa.” UTANGULIZI Asili ya kilimo cha matango inaaminika kuwa ni kaskazini magharibi mwa India ambako yamekuwa yakilimwa kwa zaidi ya miaka thelathini sasa. Hata hivyo kwa sasa, matango, hustawishwa katika sehemu nyingi za kitropiki. Matunda yake hukatwa katwa na kuliwa kama achali, au kachumbari, au huwekwa kwenye siki na pia hupikwa na kuliwa. Katika nchi yetu ya Tanzania matango hulimwa katika mikoa ifuatayo: Tanga, Morogoro, Mbeya, Lindi, Mtwara na Pwani ambako kuna jua la kutosha. Pia mikoa ya Arusha na Kilimanjaro kilimo cha matango hukubali. Aina Za Matango Zipo aina nyingi za matango lakini hutofautiana kwa umbo na rangi. Aina zinazojulika na kulimwa zaidi hapa kwetu ni: Colorad, Telegraph, Palmetto, Chicago, Pickling, Straight 8 na Mark...
"Kulingana na msimu mahindi hupandwa mwanzoni mwa mwezi wa 11 baada ya mvua za kwanza kunyesha (specifically from 1 st to 15 th day of November) ambayo huvunwa mwezi Machi mwishoni au aprili mwanzoni. Pia mahindi hupandwa mwanzoni mwa mvua za masika yaani mwezi wa pili mwishoni na mwezi wa tatu mwanzoni ambayo huvunwa mwezi Julai katikati na Agosti mwanzoni...." KUANDAA SHAMBA, KUPANDA NA KUPALILIA 1. Kuandaa Shamba, Kusafisha, Kulima/Kutifua Ni vyema mashamba yaandaliwe mapema kabla ya msimu wa kupanda haujaanza ili kumpa mkulima fursa ya kupanda kwa wakati unaotakiwa. Kuna njia mbalimbali zinazotumika kuandaa mashamba. Kati ya njia hizi ni pamoja na kufyeka, kung’oa visiki na kulima. Shamba linaweza kulimwa kwa kutumia: i). Jembe la mkono - wengi wanatumia ii). Jembe la kukokotwa na wanyama kama ng’ombe iii) . Power tillers iv). Matrekta Matumizi ya trekta, power tillers na jembe la kukokotwa na wanyama yanapunguza nguvu kazi kwani vinachimbua udongo na kuufanya kuwa tif...
Comments
Post a Comment