“Matango huwa tayari kuvunwa kuanzia siku 50 hadi 60, yaani mwezi mmoja na nusu hadi miwili baada ya kupanda, na pia matunda yanatakiwa kuwa na urefu wa sentimita 15 mpaka 20, urefu pia unaweza kutofautiana kulingana na aina ya matango yaliyopandwa.” UTANGULIZI Asili ya kilimo cha matango inaaminika kuwa ni kaskazini magharibi mwa India ambako yamekuwa yakilimwa kwa zaidi ya miaka thelathini sasa. Hata hivyo kwa sasa, matango, hustawishwa katika sehemu nyingi za kitropiki. Matunda yake hukatwa katwa na kuliwa kama achali, au kachumbari, au huwekwa kwenye siki na pia hupikwa na kuliwa. Katika nchi yetu ya Tanzania matango hulimwa katika mikoa ifuatayo: Tanga, Morogoro, Mbeya, Lindi, Mtwara na Pwani ambako kuna jua la kutosha. Pia mikoa ya Arusha na Kilimanjaro kilimo cha matango hukubali. Aina Za Matango Zipo aina nyingi za matango lakini hutofautiana kwa umbo na rangi. Aina zinazojulika na kulimwa zaidi hapa kwetu ni: Colorad, Telegraph, Palmetto, Chicago, Pickling, Straight 8 na Mark...
Comments
Post a Comment